-
Recent Posts
Recent Comments
Archives
Categories
Meta
BAADHI ya wananchi waliojitokeza katika Mkutano wa hadhara wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akihutubia.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akisalimiana na Dk Maua Daftari alipowasili viwanja vya Bandataka, Chakechake kwa ajili ya kuwashukuru wanaCCM wa visiwa vya Pemba.
MAMA Mwanamwema Shein pamoja na Dk Maua Daftari pia walikuwepo katika mkutano uliofanyika Bandataka.
Mrembo wa Brazil ambaye awali alikuwa akishikilia rekodi ya dunia ya kuwa na matiti makubwa kuliko wanawake wote duniani na baadae matiti hayo kukatwa ili kuokoa maisha yake, amejaribu kujiua kwa mara ya pili akisema kuwa hawezi kuishi bila ya matiti | ||
Mrembo Sheyla Hershey wa nchini Brazil ambaye mwaka jana matiti yake makubwa yalikatwa ili kunusuru maisha yake alipopatwa na maambukizi kwenye matiti yake, amejaribu kujiua kwa mara ya pili.
Sheyla alifanya operesheni nyingi za kuongeza matiti yake ili kuvunja rekodi ya kuwa na matiti makubwa kuliko wanawake wote duniani. Alifanikiwa kuvunja rekodi hiyo lakini aliipoteza rekodi hiyo mwaka jana baada ya madaktari kuamua kuyakata matiti yake ili kuyaokoa maisha yake yalipokuwa hatarini kutokana na maambukizi. Kutokana na kushindwa kuishikilia rekodi ya dunia ya matiti makubwa, mwezi uliopita Sheyla alijaribu kujiua kwa mara ya kwanza akisema kuwa hawezi kuishi bila ya matiti yake makubwa. “Bila ya matiti yangu makubwa nachukiza na nakuwa sijielewi”, alisema Sheyla ambaye anaishi Texas nchini Marekani. Sheyla alishawahi kupatiwa matibabu ya kisaikolojia kutokana na lindi la mawazo la kupoteza kitambulisho chake cha mwanamke mwenye matiti makubwa kuliko wote duniani. Jumapili wiki iliyopita, Sheyla alijaribu kujiua kwa mara ya pili kwa kumeza kiasi kikubwa cha vidonge. Sheyla ambaye ana umri wa miaka 31 bado amelazwa hospitali tangu jumapili akiwa kwenye chumba cha watu mahututi. “Madaktari hawajui ni wakati gani atazinduka, tunamuombea dua aweze kuzinduka”, alisema mumewe. |
source nifahamishe
Katika kusherehekea siku ya wapendanao duniani, mke wa rais wa Marekani, Michelle Obama amewapa wapendanao siri ya mapenzi kuwa ni ‘Si kwa wapenzi kununiana na kuwa siriasi muda wote bali ni kuchekeshana na kupeana matabasamu wakati wote. | ||
Michelle Obama amesema kuwa siri kubwa ya mapenzi ndani ya nyumba ni kuchekeana na mpenzi wako hivyo kudumisha furaha wakati wote.
Michelle Obama amesema kuwa amekuwa akiitumia njia hiyo kuyadumisha mapenzi kati yake na rais Barack Obama na kwa kweli amefanikiwa katika hilo. Ingawa ndoa yao imekumbwa na misukosuko mingi ya kimaisha na harakati za kisiasa, ndoa hiyo imetimiza miaka 19 sasa. Bi Obama alisema kuwa siri kubwa ya kudumu kwa mapenzi ndani ya ndoa yao ni kuchekeshana na kupeana matabasamu wakati wote. Katika kusherehekea siku ya wapendanao Valentine Day, Bi Obama alisema anatarajia mzee Obama atazama mfukoni na kumnunulia zawadi ya mkufu au hereni za dhahabu. source nifahamishe |
||
Crew mzigoni
source raythegreatest
Rais wa zanzibar akimpongeza Leila kati waliofanyaa vizuri katika baishara na fedha
wahitimu wa shahada ya sheria……..
Rais wa zanzibar akimpongeza mtoto wake Asha Ali Mohammed Shein aliyehitimu shahada ya law na sheria..
WANAMICHEZO wa Kikundi cha Michezo cha Watu wenye ulimavu Zanzibar wakishiriki Uzinduxzi huo. |
WASANII wa ngoma ya Benbati nao hawako nyuma katika maonesho ya Tamasha la Sauti za Busara Zanzibar wakiwa katika Uzinduzi.
WASANII hao na mambo ya asili ya Muafrika wakionesha katika uzinduzi wa Tamasha.
MSANII Mkongwe wa Zanzibar Halikuniki akiwa na Zumari kupiota wote wakiwa katika Uzinduzi huo wakipita barabara ya Malindi kuelekea katika Viwanja vya Ngome Kongwe. |
WASANII wakiwa katika maandamano ya Uzinduzi wa Tamasha wakiwa katika mavyazi ya kiasili ya Afrika wakiwa katika maandamano wakipita katika mitaa ya Michezani. |
WASANII wa Ngoma ya Kiluwa wakiwa katika maandamano ya Uzinduzi wa Tamasha la Sauti ya Busara Zanzibar.
|
source jikunbuke
Mwanamke mmoja wa nchini Kenya amekimbiwa na mumewe akidaiwa amerogwa na amelazimika kuwalea peke yake watoto wake 12 aliowazaa kufuatia mimba sita za watoto mapacha. | ||
Mama mmoja wa nchini amekimbiwa na mumewe baada ya kuzaa mara sita watoto mapacha hali iliyomfanya mumewe na ndugu zake waamini kuwa si bure bali amerogwa.
Gladys Bulinya alijifungua kwa mara ya sita watoto wawili mapacha mwaka jana lakini ujio huo wa watoto mapacha haukupokelewa vizuri na mumewe ambaye aliamua kukimbia akidai Gladys amerogwa. Kwa mujibu wa tamaduni za baadhi ya jamii za Kenya, watoto mapacha huonekana ni mkosi kwenye familia na huaminika kuwa huleta bahati mbaya na hutishia maisha ya wazazi . Gladys alijifungua mapacha wake wa kwanza mwaka 1993 baada ya kupachikwa mimba akiwa sekondari. Wazazi wake waliwakataa watoto hao na kumlazimisha Gladys awatelekeze hospitalini. Mpenzi wa Gladys alikubali kuwachukua watoto hao na kuanza kuwalea tangu wakati huo hadi leo. Gladys aliozeshwa kwa mwanaume mwingine mzee kutoka mji mwingine ili kuficha aibu ya familia. Gladys alizaa mara tano na mara zote alikuwa akijifungua watoto wawili mapacha. Baada ya kujifungua kwa mara ya sita watoto mapacha, mume wake naye aliamua kuingia mitini na kumtelekeza Gladys akiwa na watoto wake 10 aliokuwa akiishi nao. Gladys mbali ya kukimbiwa na mumewe ametengwa pia na familia yake akionekana kuwa amerogwa. Anaendeleza maisha yake kwa kazi za kubangaiza za kutafuta chakula cha kuwalisha watoto wake. Miaka na majina ya watoto mapacha wa Gladys: 1993: John na James walizaliwa source nifahamishe |